WAANDAAJI wa shindano la kumsaka Redd’s Miss Kigamboni City 2012
 wameomba wasichana wenye sifa zinazostahili kujitokeza kushiriki katika
 shindano hilo.
Mratibu wa Redd’s Miss Kigamboni City, Somoe Ng’itu, alisema jijini 
Dar es Salaam jana kwamba tayari baadhi ya warembo wanaotarajiwa 
kushiriki shindano hilo wameanza mazoezi, lakini bado wanakaribisha 
wasichana wengine.
“Ndiyo kwanza tumeanza mazoezi juzi katika ukumbi wa Break Point 
katikati ya jiji la Dar es Salaam, lakini milango iko wazi kwa wasichana
 wengine kujitokeza ili kuleta ushindani kwenye shindano letu,” alisema 
Somoe.
Aliongeza kuwa maandalizi ya shindano hilo yanaendelea vema, ambalo 
litakalofanyika Juni 15 kwenye Ukumbi wa Navy Beach Kigamboni yanakwenda
 vema. Warembo hao wanafanya mazoezi chini ya Hawa Ismail ambaye alikuwa
 mshindi ya shindano la Kanda ya Temeke 2003.
  Somoe, aliwataja warembo ambao wameshaanza mazoezi kuwa ni pamoja na 
Caroline Peter, Theopisther Wenso, Sophia Martime, Amina Aboubakar, 
Aisha Rajab, Rosemary Peter, Mariam Mbulilo, Julieth Phili na Doreen 
Kweka.
  Aliwataja wadhamini ambao tayari wamethibitisha kudhamini shindano 
hilo kuwa ni pamoja na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), kupitia kinywaji 
chake cha Redd’s Origal, Dodoma Wine na NSSF.
No comments:
Post a Comment