Saturday, May 26, 2012

Warembo wakaribishwa Redd’s Miss Kigamboni City

WAANDAAJI wa shindano la kumsaka Redd’s Miss Kigamboni City 2012 wameomba wasichana wenye sifa zinazostahili kujitokeza kushiriki katika shindano hilo.

Mratibu wa Redd’s Miss Kigamboni City, Somoe Ng’itu, alisema jijini Dar es Salaam jana kwamba tayari baadhi ya warembo wanaotarajiwa kushiriki shindano hilo wameanza mazoezi, lakini bado wanakaribisha wasichana wengine.

“Ndiyo kwanza tumeanza mazoezi juzi katika ukumbi wa Break Point katikati ya jiji la Dar es Salaam, lakini milango iko wazi kwa wasichana wengine kujitokeza ili kuleta ushindani kwenye shindano letu,” alisema Somoe.

Aliongeza kuwa maandalizi ya shindano hilo yanaendelea vema, ambalo litakalofanyika Juni 15 kwenye Ukumbi wa Navy Beach Kigamboni yanakwenda vema. Warembo hao wanafanya mazoezi chini ya Hawa Ismail ambaye alikuwa mshindi ya shindano la Kanda ya Temeke 2003.
Somoe, aliwataja warembo ambao wameshaanza mazoezi kuwa ni pamoja na Caroline Peter, Theopisther Wenso, Sophia Martime, Amina Aboubakar, Aisha Rajab, Rosemary Peter, Mariam Mbulilo, Julieth Phili na Doreen Kweka.
Aliwataja wadhamini ambao tayari wamethibitisha kudhamini shindano hilo kuwa ni pamoja na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), kupitia kinywaji chake cha Redd’s Origal, Dodoma Wine na NSSF.

No comments:

Post a Comment