Monday, May 28, 2012

Uzinduzi Manowari Taarab Mei 30

KUNDI la muziki wa taarabu la Manowari Modern Taarab linatarajia kufanya uzinduzi wa kundi na albamu yao kwenye Ukumbi wa Hoteli ya Traventine, Magomeni jijini Dar es Salaam, Jumatano ya Mei 30 .

Msemaji wa kundi hilo, Maliki Kizo, alisema jana kwamba wamejipanga vema kuhakikisha uzinduzi huo unafana kwa kuimba nyimbo zao mpya walizorekodi katika ubora wa hali ya juu.

Alisema, kundi hilo ambalo lilianzishwa mwaka 2008 likipiga zaidi taarabu ya kiasili, limejipanga kuhakikisha linaleta mapinduzi na kuwapa raha ya kutosha mashabiki wa muziki huo.

Alizitaja nyimbo zilizopo katika albamu yao ya kwanza iitwayo ‘Sogea Nikwambie’ ni pamoja na ‘Sogea Nikwambie’ iliyobeba jina la albamu, ‘Sigara Kali’, ‘Shani’, ‘Najuta Kukufahamu’, ‘Kawaambie Wenzako’, ‘Vipi penzi liwe Uadui’, ‘Mwanzo wa Yote’ na ‘Hawajui Twapendana’.
Wasanii wanaounda kundi hilo ni pamoja na aliyewahi kuwa nyota wa muziki wa Kizazi kipya, Ally Com, Abdi Omari, Samiu Issa, Sophia Saleh, Shamim Hassan, Sauda Adam, Christina Matosi, Amina Salim na Sina Hassan. Kundi la muziki wa dansi la Chuchu Sound linatarajiwa kusindikiza uzinduzi huo.

No comments:

Post a Comment