SHINDANO la kumsaka Redd’s Miss Dar Intercollege 2012 
linatarajiwa kufanyika kwenye ukumbi wa Sunciro, ulipo Sinza Shekilango 
jijini Dar es Salaam Juni 8 mwaka huu.
Mratibu wa Shindano hilo, Dina Ismail, alisema jijini Dar es Salaam 
jana kwamba warembo watakaoshiriki shindano hilo wanaendelea na mazoezi 
kwenye hoteli ya Lamada jijini chini ya ukufunzi wa Marylidya Boniface, 
huku kwa upande wa shoo wakinolewa na Bob Rich.
Alisema, hadi sasa warembo 12 kutoka vyuo vya Biashara (CBE), Uandishi
 wa Habari (DSJ), na Time, Ustawi wa Jamii na kile cha Usimamizi wa 
Fedha (IFM), wameisharipoti kambini.
Dina, aliwataja warembo hao kuwa ni pamoja na Hilda Edward, Nancy 
Maganga, Saada Seleman, Neema 
Nashon, Rose Muchunguzi, Fina Revocatus, 
Jane Augustino, Theresia Isaya na Natasha Deo. Taji la kitongoji hicho 
linashikiliwa na Rose Msuya kutoka IFM.
Kwa upande mwingine, mratibu huyo ameziomba kampuni mbalimbali 
kujitokeza kudhamini shindano hilo, ambalo linatarajiwa kuwa la aina 
yake na hasa ikizingatiwa kuwa washiriki wake wana vigezo vya hali ya 
juu.
“Tunaomba makampuni mbalimbali yajitokeze kudhamini shindano 
letu…mpaka sasa wadhamini tulionao ni pamoja na kampuni ya Bia Tanzania 
(TBL), kupitia bia ya Redd’s Original, Lamada Hotel, Ndege Insurance, 
Dodoma Wine na Clouds Fm.
No comments:
Post a Comment