Tuesday, May 29, 2012

Redd’s Miss Dar Intercollege Juni 8

SHINDANO la kumsaka Redd’s Miss Dar Intercollege 2012 linatarajiwa kufanyika kwenye ukumbi wa Sunciro, ulipo Sinza Shekilango jijini Dar es Salaam Juni 8 mwaka huu.

Mratibu wa Shindano hilo, Dina Ismail, alisema jijini Dar es Salaam jana kwamba warembo watakaoshiriki shindano hilo wanaendelea na mazoezi kwenye hoteli ya Lamada jijini chini ya ukufunzi wa Marylidya Boniface, huku kwa upande wa shoo wakinolewa na Bob Rich.

Alisema, hadi sasa warembo 12 kutoka vyuo vya Biashara (CBE), Uandishi wa Habari (DSJ), na Time, Ustawi wa Jamii na kile cha Usimamizi wa Fedha (IFM), wameisharipoti kambini.
Dina, aliwataja warembo hao kuwa ni pamoja na Hilda Edward, Nancy Maganga, Saada Seleman, Neema 
Nashon, Rose Muchunguzi, Fina Revocatus, Jane Augustino, Theresia Isaya na Natasha Deo. Taji la kitongoji hicho linashikiliwa na Rose Msuya kutoka IFM.

Kwa upande mwingine, mratibu huyo ameziomba kampuni mbalimbali kujitokeza kudhamini shindano hilo, ambalo linatarajiwa kuwa la aina yake na hasa ikizingatiwa kuwa washiriki wake wana vigezo vya hali ya juu.
“Tunaomba makampuni mbalimbali yajitokeze kudhamini shindano letu…mpaka sasa wadhamini tulionao ni pamoja na kampuni ya Bia Tanzania (TBL), kupitia bia ya Redd’s Original, Lamada Hotel, Ndege Insurance, Dodoma Wine na Clouds Fm.

No comments:

Post a Comment