KUNDI zima la muziki wa bongo fleva TMK Wanaume Family lenye 
maskani yakeTemeke jijini Dar es Salaam, litasindikiza utambulisho wa 
msanii chipukizi wa muziki huo Aslahi Isihaka ‘Dogo Aslay’ 
litakalofanyika Juni 9 mwaka huu kwenye Uwanja wa Jamhuri Dodoma na 
baadaye Ukumbi wa Royal Village mjini humo.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi jijini Dar es Salaam jana 
mratibu wa onesho hilo Jackline Masano wa Kampuni ya Ruhazi Promotion ya
 jijini Dar es Salaam, alisema kuwa TMK Family wamepatia kutoa burudani 
ya uhakika katika onesho hilo.
Alisema TMK Family wataungana na  wasanii kutoka kituo cha Mkubwa na 
Wanawe cha Temeke Sandali jijini katika kumsindikiza msanii huyo aliye 
gumzo hivi sasa kutokana na wimbo wake ‘Naenda Kusema’.
“Tunawaomba mashabiki na  wapenzi wa muziki huo  mjini Dodoma na 
maeneo jirani kwamba kujitokeza kwa wingi kwenye Uwanja wa Jamhuri 
kuanzia saa 6:00 mchana mpaka saa 12:00 jioni, na kisha kwenye Ukumbi wa
 Royal Village kuanzia 2:00 usiku hadi saa 6:30 ,” alisema Jackline.
Jackline aliongeza kuwa pamoja na onesho hilo kupambwa na wasanii 
wengi lakini kiingilio kitakuwa shilingi 5,000 tu kwa wakubwa na 
shilingi 1,000 kwa watoto ili kuwawezesha wapenzi wengi zaidi kukimudu 
ambapo watapata burudani ya uhakika.
Aidha, Jaqueline aliongeza kuwa kampuni yao inaendelea na mazungumzo 
na  wasanii wengine ili kuweza kusindikiza  maonesho hayo yote na pindi 
mazungumzo yatakapokamilika watawaweka hadharani.
No comments:
Post a Comment