Tuesday, May 29, 2012

TMK Family kumsindikiza Dogo Aslay

KUNDI zima la muziki wa bongo fleva TMK Wanaume Family lenye maskani yakeTemeke jijini Dar es Salaam, litasindikiza utambulisho wa msanii chipukizi wa muziki huo Aslahi Isihaka ‘Dogo Aslay’ litakalofanyika Juni 9 mwaka huu kwenye Uwanja wa Jamhuri Dodoma na baadaye Ukumbi wa Royal Village mjini humo.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi jijini Dar es Salaam jana mratibu wa onesho hilo Jackline Masano wa Kampuni ya Ruhazi Promotion ya jijini Dar es Salaam, alisema kuwa TMK Family wamepatia kutoa burudani ya uhakika katika onesho hilo.

Alisema TMK Family wataungana na wasanii kutoka kituo cha Mkubwa na Wanawe cha Temeke Sandali jijini katika kumsindikiza msanii huyo aliye gumzo hivi sasa kutokana na wimbo wake ‘Naenda Kusema’.

“Tunawaomba mashabiki na wapenzi wa muziki huo mjini Dodoma na maeneo jirani kwamba kujitokeza kwa wingi kwenye Uwanja wa Jamhuri kuanzia saa 6:00 mchana mpaka saa 12:00 jioni, na kisha kwenye Ukumbi wa Royal Village kuanzia 2:00 usiku hadi saa 6:30 ,” alisema Jackline.

Jackline aliongeza kuwa pamoja na onesho hilo kupambwa na wasanii wengi lakini kiingilio kitakuwa shilingi 5,000 tu kwa wakubwa na shilingi 1,000 kwa watoto ili kuwawezesha wapenzi wengi zaidi kukimudu ambapo watapata burudani ya uhakika.
Aidha, Jaqueline aliongeza kuwa kampuni yao inaendelea na mazungumzo na wasanii wengine ili kuweza kusindikiza maonesho hayo yote na pindi mazungumzo yatakapokamilika watawaweka hadharani.

No comments:

Post a Comment