WASANII wa muziki nchini, wametakiwa kuiga mipangilio ya
maendeleo kutoka nchini Ghana, ili kufikia mafanikio na kuachana na
vilio vya kuibiwa kazi zao kila siku.
Akizungumza na waandishi wa habari juzi, Mkurugenzi Msaidizi wa Rulu
Arts Promotions, Angelu Luhala, alisema Ghana wamejipanga vilivyo
kudhibiti wizi wa kazi za wanamuziki na kwa asilimia kubwa wamefanikiwa.
Luhala alikuwa nchini Ghana kwa mwaliko wa Kampuni ya Best AC ambayo
inashirikiana na Rulu Arts, ambako pamoja na mambo mengine, alijionea
mifumo makini ya kudhibiti wizi wa kazi za wanamuziki.
Alisema Ghana wamefanikiwa kimuziki kwa sababu wanamuziki wake wana umoja wa kweli, na serikali inawapa sapoti kubwa.
Aidha, Luhala alisema Serikali ya Ghana imekuwa ikitenga Euro milioni 2
kila mwaka kwa ajili ya utafiti katika sekta ya muziki kama moja ya
maeneo yanayoweza kutoa ajira kwa vijana na jamii kwa ujumla.
Luhala alisema serikali ya Ghana imeunda vyama vinne ambavyo
vinasaidia wanamuziki ambavyo ni pamoja na GAPI kinachohusika na
uzalishaji, usimamizi na usambazaji wa kazi za wanamuziki na GAMRO
inayohusika na ukusanyaji wa mirabaha katika kumbi za muziki, vituo vya
redio, magari na maonesho ya majukwaani.
Chama kingine ni MUSIGA ambacho wanamuziki wanafanikiwa kupitia sheria
namba 690 ya mwaka 2005 inayounda ofisi ya hakimiliki na utawala wa
hakimiliki na timu ya kudhibiti kazi za wanamuziki wakiwemo wanasheria,
polisi, wapelelezi na wanamuziki.
Na na Khadija Kalili wa Tanzania Daima
No comments:
Post a Comment