Msanii Diamond
Alisema kuwa jumla ya warembo 20 kutoka vitongoji vinne vya mkoa wa Arusha wameingiaa kambini kujiandaa na shindano hilo. Alisema warembo hao ni washindi wa kutoka vitongoji vya Miss Arusha City Centre, Njiro, Sakina na Monduli.
"Kwa kweli sio kama najisifu ila warembo wetu ni wazuri na nina imani watashinda maana wana upeo, elimu ya kutosha na maadalizi ni mazuri.
"Kingine kikubwa mwaka huu ni kwamba mashindano haya yatakuwa tofauti sana kwani tumejipanga vilivyo na hatutaki kufanya makosa.
Kwanini kila siku taji liende Dar na Mwanza tu, safari hii nitahakikisha linakuja Arusha," alisema Mwandago.
Aliwataja wadhamini wa shindano hilo kuwa ni TBL, Dodoma Wine, Tanzanite One, Mogaben Priters, Libeneke la Kaskazini blog na Arusha Traveling Lodge ambao ndio wametoa kambi ya warembo.
No comments:
Post a Comment