Sunday, June 17, 2012

Mrusi amkimbia Matumla Moshi

BONDIA wa Urusi, Vitaly Shemetov maarufu kama ‘Siberian Tiger’ ameingia mitini yeye na kocha wake kuja nchini kupambana na mkongwe, Rashid Matumla ‘Snake Man’.

Shemetov na kocha wake, walitumiwa tiketi za ndege ya shirika la Kirusi la Aeroflot, ili kuja nchini kwa ajili ya pambano hilo litakalorindima Juni 24 mjini Moshi, wakati wa Mbio za Mount Kilimanjaro.
Kwa mujibu Rais wa Shirikisho la Ngumi la Kimataifa Afrika (IBF), Onesmo Ngowi, hii ni mara ya kwanza kwa pambano la kimataifa lilioandaliwa kwa fedha nyingi, kutofanyika baada ya bondia huyo kuingia mitini kwa madai ya woga.

Ngowi alisema, Matumla ana rekodi ambayo hadi sasa hakuna bondia yeyote wa Kitanzania aliyeweza kuifikia.
“Matumla ameshawahi kuwa bingwa wa Taifa, Afrika Mashariki na Kati, Bara la Afrika, mabara na dunia aliyetambuliwa na Umoja wa Ngumi Duniani (WBU),” alisema Ngowi na kuongeza; akiwa chini ya DJB Promotions, bondia huyo ambaye kwa sasa ndiye Kamishna wa TPBC kanda maalumu ya Dar es Salaam, alionyesha alionesha kiwango cha hali ya juu.

No comments:

Post a Comment