Sunday, June 17, 2012

LISA NDIYE MISS TANZANIA 2012

KIMWANA Lisa Jensen usiku huu ameibuka kinara katika shindano maalum la kumsaka mwakilishi wa Tanzania katka shindano la Miss World mwaka huu, lililofanyika kwenye ukumbi wa 327, Mikocheni, Dar es Salaam.
 
Shindano hilo, lililoshirikisha washiriki wa zamani wa Miss Tanzania ambao hawajawahi kushinda, dalili za Lisa kushinda zilionekana tangu mwanzo, kutokana na kuwafunika washiriki ‘ile mbayaaa’ washiriki wenzake tisa.
Shindano hilo, lilianzia kwa warembo kucheza shoo ya ufunguzi kama ilivyo ada ya mashindano ya Miss Tanzania, baadaye wakapita na vazi la ubunifu, ufukweni na kumalizia na vazi la jioni, ambako kote Miss Mara wa 2006 alifunika mbaya.
Jaji Mkuu wakitangaza top 5
 
Aliyemfuatia Lisa ni Hamisa Hassan kutoka Kinondoni, wakati mshindi wa tatu alikuwa ni Pendo Laiser Miss Arusha 2008 na wengine walioingia tano bora ni Stella Mbuge na Jennifer Kakolaki.
Washiriki wengine ni Glorybayanca Mayowa, Queen Issa, Christine William, Mwajabu Juma na Neema Saleh.
 
Shindano hili, linafanyika kufuatia kalenda ya mashindano ya Miss Tanzania kubadilika na washindi wa mashindano ya mwaka huu ngazi ya awali watashiriki katika shindano la Miss Tanzania baadaye mwaka huu, kumpata mwakilishi wa Miss World mwakani.

Warembo shoo ya ufunguzi

Lisa akipongezwa na Salha, Miss Tanzania 2011 baada ya kuvikwa taji

Majaji wakipiga hesabu

Waalikwa
Sura za furaha
Glory na rafiki zake
Waalikwa
Top three
Mwaaa! hongera mama, Salha akimvisha taji Lissa

No comments:

Post a Comment