KIMWANA
Lisa Jensen usiku huu ameibuka kinara katika shindano maalum la kumsaka
mwakilishi wa Tanzania katka shindano la Miss World mwaka huu,
lililofanyika kwenye ukumbi wa 327, Mikocheni, Dar es Salaam.
Shindano
hilo, lililoshirikisha washiriki wa zamani wa Miss Tanzania ambao
hawajawahi kushinda, dalili za Lisa kushinda zilionekana tangu mwanzo,
kutokana na kuwafunika washiriki ‘ile mbayaaa’ washiriki wenzake tisa.
Shindano
hilo, lilianzia kwa warembo kucheza shoo ya ufunguzi kama ilivyo ada ya
mashindano ya Miss Tanzania, baadaye wakapita na vazi la ubunifu,
ufukweni na kumalizia na vazi la jioni, ambako kote Miss Mara wa 2006
alifunika mbaya.
 |
Jaji Mkuu wakitangaza top 5 |
Aliyemfuatia
Lisa ni Hamisa Hassan kutoka Kinondoni, wakati mshindi wa tatu alikuwa
ni Pendo Laiser Miss Arusha 2008 na wengine walioingia tano bora ni
Stella Mbuge na Jennifer Kakolaki.
Washiriki wengine ni Glorybayanca Mayowa, Queen Issa, Christine William, Mwajabu Juma na Neema Saleh.
Shindano
hili, linafanyika kufuatia kalenda ya mashindano ya Miss Tanzania
kubadilika na washindi wa mashindano ya mwaka huu ngazi ya awali
watashiriki katika shindano la Miss Tanzania baadaye mwaka huu, kumpata
mwakilishi wa Miss World mwakani.
 |
Warembo shoo ya ufunguzi |
 |
Lisa akipongezwa na Salha, Miss Tanzania 2011 baada ya kuvikwa taji |
 |
Majaji wakipiga hesabu |
 |
Waalikwa |
 |
Sura za furaha |
 |
Glory na rafiki zake |
 |
Waalikwa |
 |
Top three |
 |
Mwaaa! hongera mama, Salha akimvisha taji Lissa |
No comments:
Post a Comment