Miss Kigamboni 2012, Edda Sylvester (katikati) 
akiwa na mshindi wa pili Agnes Goodluck (kushoto) na mshindi wa tatu 
Elizabeth Boniphace mara baada ya kutangwazwa washindi.
Edda Silyvester, 21, ambaye ni mwanafunzi wa shahada
 ya kwanza katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam sehemu ya Mlimani alitwaa
 taji la Miss Kigamboni katika shindano lililofanyika kwenye ukumbi wa 
Navy Beach usiku wa kuamkia jana, na kuingia hatua ya Kanda akiongoza 
wasichana wengine wanne.
Jaji mkuu wa shindano hilo, Benny Kisaka, 
alitangaza kuwa badala ya warembo watatu, watachukua warembo washindi 
watano wa kwanza miongoni mwa washiriki tisa kuingia shindano la Kanda 
ya Temeke baadaye mwaka huu.
Kutokana na ushindi huo Edda alizawadiwa 
Sh.500,000 taslimu na mgeni rasmi katika shindano hilo, diwani wa Kata 
ya Kigamboni, Dotto Msawa.Nafasi ya pili katika shindano hilo 
lililopambwa na burudani safi kutoka bendi ya FM Academia 'Wazee wa 
Ngwasuma' ilichukuliwa na Agnes Goodluck ambaye alipata zawadi ya 
Sh.350,000.
Elizabeth Boniface alichaguliwa kuwa 
mshindi wa tatu na kupata zawadi ya Sh.300,000. Esther Albert na Khadija
 Kombo walishika nafasi za nne na tano na kila mmoja alipata zawadi ya 
Sh.200,000.
Warembo wengine walioshiriki shindano hilo
 walikuwa ni Sophia Martin, Rosemary Peter, Doreen Kweka na Linnah David
 waliopewa kifuta jasho cha Sh.150,000 kila mmoja.
Wakati huo huo, Matlda Martine alitwaa taji la Miss Dar City Centre katika shindano lingine lililofanyika jijini juzi usiku pia.
No comments:
Post a Comment