Monday, June 18, 2012

Msomi UDSM awa Miss Kigamboni


Miss Kigamboni 2012, Edda Sylvester (katikati) akiwa na mshindi wa pili Agnes Goodluck (kushoto) na mshindi wa tatu Elizabeth Boniphace mara baada ya kutangwazwa washindi.
Edda Silyvester, 21, ambaye ni mwanafunzi wa shahada ya kwanza katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam sehemu ya Mlimani alitwaa taji la Miss Kigamboni katika shindano lililofanyika kwenye ukumbi wa Navy Beach usiku wa kuamkia jana, na kuingia hatua ya Kanda akiongoza wasichana wengine wanne.
Jaji mkuu wa shindano hilo, Benny Kisaka, alitangaza kuwa badala ya warembo watatu, watachukua warembo washindi watano wa kwanza miongoni mwa washiriki tisa kuingia shindano la Kanda ya Temeke baadaye mwaka huu.
Kutokana na ushindi huo Edda alizawadiwa Sh.500,000 taslimu na mgeni rasmi katika shindano hilo, diwani wa Kata ya Kigamboni, Dotto Msawa.Nafasi ya pili katika shindano hilo lililopambwa na burudani safi kutoka bendi ya FM Academia 'Wazee wa Ngwasuma' ilichukuliwa na Agnes Goodluck ambaye alipata zawadi ya Sh.350,000.
Elizabeth Boniface alichaguliwa kuwa mshindi wa tatu na kupata zawadi ya Sh.300,000. Esther Albert na Khadija Kombo walishika nafasi za nne na tano na kila mmoja alipata zawadi ya Sh.200,000.
Warembo wengine walioshiriki shindano hilo walikuwa ni Sophia Martin, Rosemary Peter, Doreen Kweka na Linnah David waliopewa kifuta jasho cha Sh.150,000 kila mmoja.
Wakati huo huo, Matlda Martine alitwaa taji la Miss Dar City Centre katika shindano lingine lililofanyika jijini juzi usiku pia.

No comments:

Post a Comment